
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Kiongozi wa Muungano wa Upinzani, Nasa, nchini Kenya, Raila Odinga, amepuuzia uchaguzi wa marudio wa Urais uliofanyika jana nchini humo na kudai kwamba haukuwa wa halali, hivyo anajiandaa kwa uchaguzi mwingine.
Odinga amesema, uchaguzi huo haukuwakilisha Wakenya walio wengi hivyo yeye anajiandaa kwa uchaguzi mwingine utakaofanyika baada ya siku 90.
Akizungumza kwa mara ya kwanza tangu kufanyika kwa uchaguzi huo wa marudio, Odinga amesema kwamba uchaguzi huo mwingine utafanyika hata kama malalamiko yao hayatashughulikiwa na Tume ya Uchaguzi IEBC.
Odinga amesisitiza kwamba, muungano wa upinzani, hauutambui uchaguzi huo wa marudio kufuatia kuvurugika katika baadhi ya maeneo nchini humo.
Odinga aliamua kujitoa kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi siku chache kabla ya kufanyika kwa uchaguzi huo wa marudio uliofanyika hana Oktoba 26 baada ya ule wa Agosti 08 kutenguliwa na mahakama kwa madai kwamba ulikuwa na dosari nyingi.
Post A Comment: