
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Nahodha wa Njombe Mji, Laban Kambole amesema uzoefu mdogo wa ligi umechangia kupata kipigo cha mabao 4-0 kutoka kwa Simba jana kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.
Kambole alisema Simba ni timu kubwa tofauti na wao ambao wamepanda daraja msimu huu na kucheza Ligi Kuu kwa mara ya kwanza mwaka huu.
"Timu yetu wachezaji wengi ni wachanga na ukweli tulizidiwa katika mchezo huo kwani wengi hawana uzoefu wa ligi."
"Tatizo kubwa la wachezaji wengi wa Tanzania huwa tunaogopa majina ya hizi timu hivyo unakuta ukifika uwanjani unasahau kufanya uliyoelekezwa na kucheza unavyojua wewe," alisema Kambole.
Kambole alisema bado wana nafasi ya kufanya vizuri katika michezo mingine ijayo kwani wanachoshukuru wameshamaliza kucheza na Yanga na Simba kwenye mzunguko wa kwanza.
"Tumeshacheza na Yanga na Simba hivyo sasa tutashusha presha na kupambana katika michezo ijayo kuhakikisha haturudi tulikotoka," alisema nahodha huyo ambaye timu yake ilicheza kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Uhuru.
Post A Comment: