
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Homa ya mechi ya watani wa jadi imepanda. Simba inaondoka Dar es Salaam leo Jumatatu kwenda Zanzibar kuweka kambi lakini wenzao Yanga wanatokea Shinyanga kuelekea Morogoro.
Simba na Yanga ambazo zinacheza Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, zimeanza harakati za kuwindana kila mmoja akijiweka sawa kwa pambano hilo ambalo ni turufu muhimu kwa ubingwa.
Mratibu wa Simba, Abbas Ally alisema; "Tuna mechi ngumu dhidi ya Yanga, tutaondoka wote kuelekea Zanzibar katika kambi ya pambano la watani," alisema.
Mara ya mwisho Watani hao walikutana katika mechi ya Ngao ya Hisani ambapo Simba ilitokea Unguja na Yanga kisiwa cha Pemba na Simba kuibuka na ushindi wa penalti 4-2 baada ya kumaliza dakika 90 bila kufungana.
Habari za uhakika kutoka Shinyanga zinasema kwamba Yanga safari hii haitakwenda Zanzibar bali itakwenda kutulia Morogoro mpaka siku moja kabla ya mechi ya watani ambayo ni Ijumaa.
Post A Comment: