ads

Marekani imesema kuwa imefanikiwa kwa kiasi kikubwa katika jaribio lake la kwanza la mtambo wa kutungua makombora ya nyuklia ya masafa marefu.


Mtambo huo wa ardhini umefungwa katika kambi ya kijeshi iliyopo Califonia kwaajili ya kujihami na vitisho ambavyo vimekuwa vikitolewa na maadui zake ikiwemo Korea Kaskazini.

Aidha, Pentagon imesema kuwa jaribio hilo limefanyika baada ya Korea Kaskazini kufanya majaribio yake ya makombora tisa ya masafa marefu mwaka huu hivyo kutishia usalama wa nchi hiyo.

“Mfumo huu ni mhimu sana kwa ulinzi wa taifa letu na jaribio hili ni uthibitisho mkubwa kwamba tuna uwezo wa hali ya juu wa kujilinda na kutetea usalama wa raia wetu,” amesema Mkurugenzi wa kitengo cha ulinzi wa makombora, Admirali Jim Syring.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: