ads

Hali ya sintofahamu imekikumba chama cha ACT-Wazalendo baada ya Mwenyekiti wa chama hicho kuteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. John Magufuli kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro.


Hayo yametokea mara baada ya Afisa Habari wa chama hicho, Abbdallah Khamis kushindwa kuelezea undani wa tukio hilo huku ikisemekana baadhi ya wanachama kutoa shinikizo la kukataa uteuzi huo alioteuliwa na Rais.

“Uteuzi huo hata sisi tumeusikia kwenye vyombo vya habari, hivyo chama kitakaa kikao na Mwenyekiti wetu ili tuweze kuzungumza nae, kani kwasasa siwezi kuzungumzia chochote kwasababu muhusika yupo safarini, hata Zitto naye kasikia kwenye vyombo vya habari hivyo baada ya kikao chama kitatoa tamko,”amesema

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: