ads

Simu moja aina ya smartphone imechukua jukumu muhimu katika majaribio ambayo huenda yakasaidia mamilioni ya watu duniani ambao wanakabiliwa na ugonjwa wa kisukari ili kuweza kuthibti kiwango cha sukari.


Watafiti wa China katika jarida la sayansi wanasema walivumbua seli za insulini na kuzidunga ndani ya panya ili kufanya kazi wakati zinapoangazwa na mwanga wa LED.

Mwanga huo ulizalishwa na programu ya simu hiyo aina ya smartphone baada ya kupokea data kutoka kwa kifaa cha kupimia damu ilio na sukari ndani ya panya huyo.

Kwa sasa watu walio na kisukari hupimwa damu ili kubaini ni wakati gani wanahitaji sindano za insulini.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: