ads

Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi, Mwigulu Nchemba amesisitiza kuwa changamoto ya mauji ya watu mkoani Pwani iko mbioni kutatuliwa kwa kuwa serikali imeshabaini wanaofanya mauaji hayo ni watu wanaotoka kwenye maeneo ya Kitibi, Mkuranga na Rufiji.


Mwigulu aliyasema hayo leo Bungeni mjini Dodoma wakati akitoa maelezo juu ya matukio yanayoendelea mkoa wa Pwani.

Alisema kuwa kamata kamata itaendelea katika wilaya za Kibiti, Mkuranga na Rufiji hadi wahalifu wote watakapokamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola.

Awali Mbunge wa Rombo, Joseph Selasini aliomba Bunge liahirishe shughuli zake ili kujadili hali ya amani katika maeneo hayo.

"Kwa sasa watu wanakamatwa hovyo na polisi katika maeneo hayo na mfano kijana Sultan Mpigi aliyekamatwa na polisi akiwa mzima lakini maiti yake ilikutwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili". Alisema Selasini.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: