ads

Kesi ya unyang’anyi wa kutumia silaha na kujeruhi inayomkabili Salum Njetwe maarufu ‘Scorpion’ imeshindwa kuendelea kusikilizwa kwa mara ya nne mfululizo baada ya wakili wa utetezi kushindwa kufika mahakamani.


Wakili huyo, Juma Nassoro ameshindwa kufika leo, Alhamisi katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala kwa ajili ya kumtetea mteja wake, baada ya kuwa na kesi nyingine Mahakama Kuu.

Wakili  Mwandamizi wa Serikali, Nassoro Katuga ameiambia Mahakama kuwa alipewa taarifa na wakili huyo kuwa alikuwa na kesi nyingine Mahakama kuu kwa Jaji Wambura.

“Mheshimiwa hakimu,  mshtakiwa yupo mbele ya mahakama yako lakini nimepata taarifa kutoka kwa wakili wake kuwa yupo Mahakama Kuu kwa Jaji Wambura mbapo anasikiliza kesi , hivyo tunaiomba Mahakama yako itoe ahirisho la mwisho na kupanga tarehe nyingine kwa ajili ya  kuendelea na ushahidi”Alidai Katuga.

Hakimu  Mkazi  Flora Haule , anayesikiliza shauri hilo amekubalia ombi la upande wa mashtaka na kuahirisha kesi hiyo hadi Juni 8, mwaka huu na mshtakiwa amerudishwa rumande kutokana na shtaka linalomkabili kutokuwa na dhamana kwa mujibu wa sheria.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: