ads

MTOTO wa darasa la kwanza katika shule ya msingi Ubena, Tarafa ya Chalinze mkoa wa Pwani aliyefahamika kwa majina ya Karim Salum, anasadikika kufariki dunia baada ya kuzama kwenye maji ya mto Ngerengere wakati akiogelea na wenzake huku jitihada za kutafuta mwili wake zikigonga mwamba kutokana na wananchi kuutafuta mwili huo kwa zaidi ya siku mbili mfululizo bila mafanikio.


Chanzo kimeshuhudia wananchi wakiendelea na jitihada za utafutaji wa mwili wa mtoto Karim Salum anayesadikiwa kufa maji huku vijana walioshuhudia mtoto huyo akizama ndani ya maji wakieleza tukio hilo lilitokea majira ya saa kumi Alasiri wakati wakijaribu kuogelea ndani ya mto huo.

Naye Babu wa mtoto huyo Bwana Issa Bung’ombe ameeleza kusikitishwa na tukio hilo na kwamba mtoto huyo aliaga nyumbani akielekea mtoni kuchota maji ndipo kadhia hiyo ilipomkuta.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: