ads

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume ya Uchaguzi (NEC) Ramadhan Kailima amewataka wananchi wasikubali kumpa kadi ya kupigia kura mtu yeyote isipokuwa kuionyesha kwenye kituo cha kupigia kura siku ya uchaguzi.


Sambamba na hilo, Kailima amewaambia waandishi wa habari kuwa ACT-Wazalendo na vyama vingine vya siasa vyenye wagombea katika uchaguzi mdogo wa madiwani na ubunge, kutumia haki zao kuwasilisha malalamiko ya ukiukwaji wa maadili kwa kamati husika.

“Kwa kuzingatia sehemu ya 5.4 ya maadili ya uchaguzi, Tume inavikumbusha vyama vya siasa kuwasilisha malalamiko yao katika kamati ya maadili ngazi ya kata ndani ya saa 72 tangu kutokea kwa ukiukwaji wa maadili,”amesema Kailima.

Amesema kama chama hakitaridhika na uamuzi utakaotolewa na kamati ya maadili ngazi ya kata, kwa kuzingatia sehemu ya 5.7(a) ya maadili ya uchaguzi awasilishe rufaa kwa msimamizi wa uchaguzi ngazi ya jimbo ndani ya saa 24 tangu uamuzi wa ngazi ya kamati ya kata kutolewa.

Kailima amesema endapo chama bado hakijaridhika na uamuzi ya ngazi ya jimbo, kwa kuzingatia sehemu ya 5.7(b) na (c), kina fursa ya kuwasilisha rufaa kamati ya maadili ya ngazi ya taifa au ngazi ya rufaa ambayo ni NEC.

“Kwa mujibu sehemu ya 5.7(e) ya maadili ya uchaguzi, kama chama au mgombea hakuridhika na uamuzi ya kamati ya rufaa atakuwa na fursa ya kuwasilisha malalamiko yake mahakamani baada ya uchaguzi kufanyika kwa mujibu wa Sheria ya Taifa ya Uchaguzi Sura ya 343 na Sheria ya Uchaguzi ya Serikali za Mitaa, Sura ya 292,” alisema.
DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: