ads



Bondia maarufu nchini Tanzania Francis Cheka, Jana ametangaza rasmi kustaafu mchezo wa masumbwi kwa kile alichokieleza ni ubabaishaji wa ma-promota pamoja na kutopata faida katika mchezo huo. 


Cheka ambaye anakabiliwa na tuhuma za kuchukua pesa na kugoma kupanda ulingoni katika pambano lililokuwa limeandaliwa siku ya Krismasi, amesema amechoshwa na kile alichokiita kuwa ni utapeli wa mapromota, na kwamba sasa atajikita zaidi katika mapambano ya kuhamasisha vijana.

Akiwa amedumu kwenye ndondi nchini kwa takribani miaka 19, Cheka amesema mchezo huo umetawaliwa na majungu, na fitina huku watu wengi wakifikiri kuwa kuna pesa nyingi, wakati hakuna anachokipata zaidi ya umaarufu na kuhojiwa kwenye vyombo vya habari.

"Huu mchezo una majungu na fitina, hakuna faida yoyote zaidi ya kuhojiwa na waandishi wa habari, hakuna pesa, tunapata pesa gani, watu wanadhani tunapata pesa,  nitabaki kucheza mapambano kwa ajili ya kuhamasisha vijana katika ngumi pamoja na kufanya biashara nyingine nipate pesa, nimedumu kwenye ngumi zaidi ya miaka 19, nimevumilia mengi" Amesema Cheka.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: