ads

UPELELEZI wa kesi mbili zinazomkabili Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Kampuni ya Jamii Media Limited, Mexence Melo (40), haujakamilika.


Kesi hizo zimetajwa jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Thomas Simba na Hakimu Mkazi, Geofrey Mwambapa.

Wakili Mwandamizi wa Serikali, Mohammed Salum alidai kuwa kesi hiyo imekuja kwa ajili ya kutajwa na kwamba upelelezi wake haujakamilika hivyo, aliomba tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.

Kutokana na hali hiyo, Hakimu Simba ambaye anasikiliza kesi namba 456 na Hakimu Mwambapa anayesikiliza kesi namba 457, waliahirisha kesi hiyo hadi Januari 26, 2017 na kutaka upande wa mashitaka kuhakikisha upelelezi huo unakamilika haraka.

Inadaiwa kuwa kati ya Aprili Mosi mwaka huu na Desemba 13, mwaka huu maeneo ya Mikocheni wilayani Kinondoni, mshitakiwa akiwa Mkurugenzi wa kampuni hiyo inayoendesha tovuti ya Jamii Forum, alishindwa kutoa taarifa kuhusu miliki hiyo huku akijua kwamba jeshi hilo linafanya uchunguzi wa makosa ya jinai yaliyochapishwa kielektroniki kwenye tovuti hiyo.

Pia inadaiwa mshitakiwa alizuia jeshi hilo kufanya uchunguzi kinyume na Sheria Namba 22 (2) cha Sheria ya Makosa ya Mtandao Namba 14 ya mwaka 2015.

Salum alidai kuwa kati ya Mei 10 mwaka huu na Desemba 13 mwaka huu maeneo ya Mikocheni, akiwa Mkurugenzi wa Kampuni hiyo, alilizuia jeshi hilo kufanya uchunguzi kwa kushindwa kutoa taarifa zilizochapishwa na tovuti hiyo.

Aidha, katika kesi ya tatu, mshitakiwa alikabiliwa na mashitaka mawili ikiwemo la kuendesha mtandao kwa usajili usio wa Tanzania na kuzuia jeshi kufanya uchunguzi.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: