ads

AZAM imeingia mkataba wa miaka mitatu na kocha wake wa zamani Kalimangonga ‘Kally’ Ongala kuifundisha timu hiyo.


Timu hiyo imefikia hatua hiyo baada ya kutimua benchi lote la ufundi likiongozwa na Zeben Hernandez Rodriguez. Habari za uhakika kutoka Azam zilisema jana tayari Kally yupo Dar es Salaam na kuna masuala madogo yanakamilishwa.

Kally, aliyekuwa msaidizi wa Stewart Hall Azam, kwa sasa ni kocha wa Majimaji aliyokuwa na mkataba nao wa mwaka mmoja.

Mtendaji Mkuu wa Azam, Saad Kawemba hakutaka kulizungumzia hilo jana lakini Mwenyekiti wa Majimaji Humphrey Milanzi alisema wapo kwenye mazungumzo na viongozi wa Azam juu ya kuvunja mkataba huo wa mwaka mmoja.

“Ni kweli viongozi wa Azam walitupigia simu kuhusu kumtaka Kally na sasa tunaangalia namna ya kuvunja mkataba wa mwaka mmoja tulioingia kati yetu na kocha Kally,” alisema.

Mapema jana Kawema aliwaambia waandishi wa habari kwamba timu yao itakuwa chini ya kocha wa vijana Iddi Nassor ‘Cheche’ kwa muda akisaidiwa na Iddi Abubakar.

Jopo la makocha hao wa Hispania, mbali na Hernandez wengine ni Yeray Romero, Kocha wa Makipa Jose Garcia, Kocha wa Viungo, Pablo Borges na Mtaalamu wa tiba za Viungo, Sergio Perez.

Kawemba alisema uamuzi wa kuwaondoa makocha hao umefikiwa na Bodi ya Wakurugenzi wa timu hiyo juzi, na umetokana na mwenendo mbaya wa Azam FC kwenye Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, ambayo imefikia raundi ya pili hivi sasa.

“Tunawashukuru kwa mchango wao, walitupa taji la ngao ya jamii tuliweza kuifunga Yanga kwa penalti 4-1 tunawatakia maisha mema huko waendako,” alisema.

SOURCE - Habari Leo

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: