ads

MAMBO magumu. Hatua mbalimbali zinazochukuliwa na Serikali katika kuhakikisha kuwa kila mtu anajiingizia mapato kutokana na shughuli halali na si kutegemea ‘dili’ za mjini zimeendelea kuibua vilio kutokana na ukata mkali kwa mamia ya watu.

Uchunguzi uliofanywa  kwa siku kadhaa, umebaini kuwa miongoni mwa waathirika wakubwa wa uhaba huo wa fedha zilizokuwa zikipatikana kirahisi kupitia ‘dili’ nyingi, zilizokuwapo walau mwaka jana kulinganisha na sasa, ni pamoja na wajasiriamali mbalimbali ambao sasa wamejikuta wakiwa katika hali mbaya kiuchumi.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, umebaini kuwa baadhi ya wajasiriamali wamejikuta wakifilisika baada ya biashara zao kuyumba na mwishowe kushindwa kulipa mikopo waliyoipata kutoka benki na taasisi zingine za fedha.

Hatua hiyo imesababisha kutwaliwa mali walizoziweka dhamana, zikiwamo viwanja, majengo kama ya shule na nyumba za makazi, nyumba za kulala wageni, hoteli pia magari.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  



ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: