ads

Mbunge wa Arumeru Mashariki Joshua Nassari amesema kitendo cha serikali kupeleka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kuchimba mashimo ya kuweka nguzo za umeme na kubaki hivyo bila ya nguzo na umeme kufikishwa ni kuwanawisha na kuwanyima chakula.


Mbunge Nassari ameyasema hayo Bungeni Mjini Dodoma katika mkutano unaoendea wakati wa maswali na majibu katika wizara ya Nishati na Madini.

Mheshimiwa Mwenyekiti Kuna juhudi zimefanyika huko nyuma za kupeleka umeme vijijini lakini sasa hivi jimboni kwangu kuna vijiji ambavyo REA walichimba mashimo na kuyaacha wazi wakati wananchi walifyeka mazao yao serikali haioni kwamba kitendo hiki ni sawa na kuwanawisha mikono na kuwanyima chakula, ni lini serikali itapeleka nguzo na kuwafungia wananchi hawa umeme?

Akijibu swali hilo Naibu Waziri wa Wizara ya Nishati na Madini Dkt.Medard Kalemani amesema vijiji vyote nchini ambavyo vipo katika awamu ya tatu ya mradi wa REA vitapatiwa umeme baaada ya wabunge kupitisha bajeti ya wizara hiyo na fedha kutoka kwenda kuendeleza miradi hiyo.

Dkt. Kalemani amewaondoa wasiwasi wabunge wanaopitiwa na miradi hiyo kwamba watakwenda kushughulikia kero ya umeme kuanzia mwezi wa saba 2016.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: