ads

Msanii Ommy Dimpoz ambaye kwa sasa anafanya poa na wimbo wake 'Achia boy' amefunguka na kusema kuwa ameamua kumuweka wazi mpenzi wake ili kupunguza usumbufu kutoka kwa watoto wa kike.


Akizungumza kwenye kipindi cha Planet bongo cha East Africa Radio, Ommy Dimpoz alidai kuwa kufanya hivyo ni kupunguza kasi ya watoto wa kike ambao wamekuwa wakimsumbua na kumtaka kimapenzi.

"Unajua saizi nimeamua kumuweka wazi mpenzi wangu ili wajue yupo na kupunguza usumbufu kwa watoto wa kike ambao wanadhani labda niko single, japo yupo mbali lakini kufanya hivyo inasaidia" alisema Ommy Dimpoz

Mbali na hilo Ommy Dimpoz alisema mpenzi wake huyo kwa sasa anasomea udaktari nchini uingereza na kudai ni mtu wa Afrika Mashariki.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: