ads
NYOTA wa nyimbo za Injili Bongo, Rose Muhando anadaiwa kumkimbia meneja wake, Alex Msama licha ya kuwepo kwa makubaliano kati yao yaliyohusu kulipiwa deni la kiasi cha shilingi milioni sita alizokuwa akidaiwa msanii huyo mwenye jina kubwa.
Alex Msama ambaye ni meneja wa Rose muhando.

“Meneja wake alikubali kumlipia pesa zote (6,500,000) ambazo Rose alikuwa anadaiwa baada ya kushindwa kuhudhuria tamasha moja huko mikoani, alitakiwa baada ya siku chache aingie studio kufanya kazi, lakini ametoweka na haifahamiki yupo wapi,” kilisema chanzo chetu.

Msama alipotafutwa alikiri kutokea kwa tukio hilo, akisema haeleweki Rose ana matatizo gani kwani walikubaliana baada ya siku chache aingie studio na kurekodi, lakini mpaka hivi sasa haijulikani alipo na hata simu yake ya mkononi haipatikani.
GPL
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: