Rais wa Zimbabwe, Robert Mugabe amekubali kujiuzulu nafasi ya urais wa nchi hiyo kwa masharti kuwa yeye na mkewe Grace Mugabe wapatiwe kinga ya kudumu na mali zake binafsi zisiharibiwe wakati wa maisha yake yote baada ya kujiuzulu.


Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwenye tovuti ya kituo cha runinga cha CCN zimedai kuwa Rais Mugabe ameshawasilisha masharti hayo kwa njia ya barua na tayari Jeshi la nchi hiyo limekubaliana nayo.

Wakati hayo yakifanyika kwa usiri mkubwa, Chama cha Zanu PF leo kimetangaza kukutana na wabunge, Mawaziri na Maseneta wa Chama hicho mchana huu.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: