Beki Shomari Kapombe amesema yuko tayari kama Simba watavunja mkataba.


Kapombe amesema hayo akijibu kauli ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili Simba, Zacharia Hans Poppe aliyemtaka acheze au aondoke Simba kwa kuwa hawako tayari kuendelea kumlipa bure bila kufanya kazi.

“Mimi ni majeruhi, siwezi kucheza. Kama wanaona wanataka kuvunja mkataba niko tayari.

“Asingekwenda kuzungumza kwenye vyombo vya habari, angenitafuta mimi ili kujua kinachoendelea,” alisema.

Kapombe amekuwa akiendelea na matibabu tokea ajiunge na Simba akitokea Azam Fc.

Hajapata nafasi ya kuichezea Simba jambo ambalo linaonekana kumuudhi Hans Poppe.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: