
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Ili kupunguza gharama za uendeshaji, Serikali imetangaza kuachana na matumizi ya karatasi kutoa nakala za malipo ya mshahara (salary slip) kwa watumishi wa umma.
Badala yake, Serikali sasa itaanza kutumia mfumo wa kielektroniki.
Taarifa iliyotolewa jana Jumapili na Wizara ya Fedha na Mipango, imesema watumishi wa umma wataanza kutumia mfumo huo kwenye masuala yao yote ya kiutendaji ikiwemo kukamilisha mahitaji ya taasisi za fedha watakapokuwa wakihitaji mkopo au wanaposhughulikia mafao kwenye mifuko ya hifadhi ya jamii.
Taarifa hiyo imesema hata wastaafu watapaswa kufuata utaratibu huo mpya pamoja na wadau wengine wanaoshirikiana na wafanyakazi wa umma yakiwemo mashirika ya bima.
Ili kupata nakala hiyo, maelekezo yanasema kila mtumishi au mstaafu serikalini atahitaji kujisajili.
Taarifa imesema kutokana na gharama kubwa za uchapishaji, usambazaji na usumbufu wa kuzitafuta nakala hizo, wizara imeandaa mfumo wa kielektroniki wa utoaji wa hati za malipo ya mshahara ujulikanao government salary slip self service.
Imeelezwa utaratibu wa kujisajili na kuutumia mfumo huo unatolewa na waajiri.
Post A Comment: