
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Jumla ya wanawake 187,267 wamefanyiwa uchunguzi wa saratani ya shingo ya kizazi huku 7,602 wakipatiwa matibabu katika mradi uliofadhiliwa na Taasisi ya Bill and Melinda Gates baada ya kukutwa na ugonjwa huo.
Mradi huo uliokuwapo kwa miaka mitano ulikuwa ukitekelezwa na taasisi za Marie Stopes Tanzania (MST), Chama cha Uzazi na Malezi Bora Tanzania (Umati) na PSI.
Akizungumza wakati wa kufunga mradi huo juzi, Mkurugenzi Mkazi wa MST, Anil Tambay alisema idadi hiyo ya wanawake imetoka katika mikoa 22 ambako mradi huo ulikuwa ukitekelezwa.
βMradi huu ulijikita kupunguza athari za saratani na shingo ya kizazi kwa wanawake, tumefanya uchunguzi na kutoa matibabu,β alisema Tambay.
Alifafanua kuwa wakati wa kuanza kwa mradi huo walitoa mafunzo na kupata watoa huduma 210 waliohudumia vituo 79 vilivyoanzishwa.
Kaimu Mkurugenzi wa Kitengo cha Afya ya Uzazi wa Wizara ya Afya, Dk Hussein Kidanto alisema asilimia 38 ya wagonjwa waliofika katika Taasisi ya Saratani ya Ocean Road mwaka 2015 walikuwa na saratani ya shingo ya kizazi.
Post A Comment: