
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Winga wa Timu ya Taifa Stars, Simon Msuva amesema kwamba pamoja na kutoka sare ya bao 1-1 dhidi ya timu ya Taifa ya Malawi katika mchezo wa kirafiki jana anaamini kwamba timu hiyo ilikuja kulipiza kisasi cha kipigo walichokipata katika michuanoCOSAFA iliyofanyika nchini Afrika ya Kusini lakini wameshindwa.
Akizungumza baada ya mchezo uliochezwa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam, Msuva amesema kwamba wao walikuwa wamejiandaa kwa ushindi lakini haikuwa hivyo na hatimaye kuangukia kupata sare ya bao moja ambalo alilifunga yeye mwenyewe katika dakika 57 ya mchezo .
Katika mchezo huo ambao ulijaa purukushani za kutosha ulimpelekea Kocha wa timu ya Malawi kutolewa uwanjani kwa sababu ya kuvuka mipaka ya benchi la ufundi na kuingia uwanjani wakati mechi ikiendelea.
Hata hivyo katika mchezo huo wachezaji wawili wa Taifa Stars, Erasto Nyoni na Mzamiru Yassin walitolewa kwa kadi nyekundu kutokana na makosa ya kimichezo yaliyoonekana na refa.
Kwa upande wa Malawi walitangulia kupata goli katika dakika ya 35' kupitia Nahodha wa kikosi chao Ng'ambi Robert ambapo alipofanyiwa mahojiano alisema "hajaridhishwa sana na goli alilopata kwani alitegemea kufunga magoli zaidi ya mawili"
Post A Comment: