ads

Aliyekuwa mgombea urais katika uchaguzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Ally Mayay ametoa ya moyoni kuhusu uchaguzi huo uliofanyika jana Jumamosi kwenye Ukumbi wa St Gasper mjini Dodoma.


Baada ya kumalizika kwa mchakato huo wauchaguzi uliosimamiwa na kamati ya uchaguzi chini ya Wakali Revocatus Kuuli, mgombea Mayay alifunguka na kusema "Hii ndiyo maana ya demokrasia au ambayo Fifa na CAF wanaizungumzia kila siku. Uchaguzi ulikuwa wa huru na haki na hata walioshinda walipata nafasi hiyo kwa uhalali," alisema.

"Sikufanikiwa kupata nafasi kwani kura zangu hazikutosha ila ninachoomba washindi waliopata nafasi hiyo kuendeleza soka na kuyatimiza yale ambayo waliahidi wakati wa kampeni," alisema Mayay.

Uchaguzi huo ulimalizika na Wallece Karia kuwa ndiye Rais na Michael Wambura kuwa makamu huku wakipatikana wagombea wengine 13, kutoka katika kila kanda.


ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: