ads

 Kiungo Mghana, James Kotei ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kuitumikia Simba hadi 2019, na kumaliza uvumi kuwa huenda angejiunga na watani zao Yanga.


Kotei alimaliza mkataba wa kuitumikia klabu hiyo mwezi uliopita, lakini mazungumzo ya kuongeza mkataba yalikwenda vizuri kabla ya kusaini mbele ya Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Zacharia Hans Poppe.

Akizungumza baada ya kusaini mkataba huo, Kotei alisema anajiandaa na kazi Msimbazi hasa baada ya kufanya vizuri katika miezi sita iliyopita ambapo alichezeshwa kama beki wa kati pamoja na kiungo.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: