ads

Baada ya kupata dhamana siku ya Juma tatu, kutokana na madai ya kutoa lugha chafu kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee  amedai mapambano yake juu ya watoto wa kike kupata elimu bado yanaendelea.


Mdee ametoa kauli yake hiyo kupitia mtandao wake wa kijamii wakati akiwashukuru wananchi na wadau waliopaza sauti kwa kitendo cha yeye kuwekwa chini ya ulinzi kwa zaidi ya muda uliopangwa.

"Kwa heshima kubwa niwashukuru sana wote mliopaza sauti zenu kutaka haki itendeke kwangu na kwa watoto wetu wa kike! Mapambano yanaendelea!" aliandika.

Halima Mdee aliwekwa chini ya ulinzi kwa agizo la mkuu wa wilaya ya Kinondoni Ally Happi kwa kuadai kwamba mbunge huyo alitoa maneno kukashifu na ya uchochezi katika mkutano wake wa Baraza la Wanawake CHADEMA uliofanyika katika ofisi za baraza hilo wakati akizungumza na wanahabari.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: