ads

Solomon L laizer diwani Kata ya Ngabobo Wilayani Arumeru kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo(CHADEMA) amejiuzulu hivi punde.


Katika barua yake kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Meru, Laizer anakiri kuridhishwa na kazi kubwa anayoifanya Mhe Rais Magufuli ambayo imeiletea heshima kubwa nchi yetu, na kudai kuwa kuendelea kukaa CHADEMA ni kuisaliti nafsi yake.

Awali katika mahojiano, Laizer anampongeza Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Ndg Alexander Mnyeti kwa kazi ya heshima anayoifanya na kumuomba amfikishie salamu kwa Rais Magufuli kwamba wananchi wa Ngabobo wanamuelewa sasa kuliko wakati wowote.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: