Aliyewahi kuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki na kada wa chama cha mapinduzi (CCM), Balozi Mwapachu jana tarehe 13/07/2017 ameamua kustaafu na kutoka kabisa katika Bodi ya Wakurugenzi ya kampuni inayojihusisha na uchimbaji wa madini Acacia


Acacia wamethibitisha Balozi Mwapachu kustaafu kwake na kujiondoa katika Bodi ya Wakurugenzi lakini pia wamemshukuru Balozi Mwapachu kwa muda wake wote wa miaka mitatu ambao walikuwa naye katika bodi hiyo kwani alikuwa na mchango mkubwa. 

"Tunamtakia maisha marefu , bodi ya wakurugenzi, wakurugenzi na timu ya usimamizi tunakubaliana na Balozi Mwapachu kwa maamuzi yake, ila tunashukuru kwa msaada wake kwa kampuni kwa kipindi chote tulichokuwa naye" alisema taarifa ya Acacia 

Kutokana na mabadiliko hayo Acacia wamefanya mabadiliko ya Bodi ya Wakurugenzi na sasa bodi ya ACACIA itajumlisha wanachama saba ambao watakuja kubainishwa siku za usoni. 

Siku za karibuni kampuni ya ACACIA ilidaiwa kuwepo Tanzania bila usajili wowote, na kudaiwa kufanya biashara ya madini kinyume na utaratibu na sheria za nchi kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa na tume mbili zilizoundwa na Rais John Pombe Magufuli kuchunguza madini mbalimbali ambayo yapo kwenye mchanga wa madini unaofahamika kama makinikia. 
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: