ads

Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage leo Alhamisi amevaa viatu vya Profesa Sospeter Muhongo kwa kusoma bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini bungeni.


Mwijage anavaa viatu hivyo baada ya Rais John Magufuli kutengua uteuzi wa Profesa Muhongo kama waziri wa wizara hiyo kutokana na kushindwa kusimamia vizuri wizara.

Hilo lilitokea baada ya Rais Magufuli kupokea ripoti ya kamati ya kwanza ya kuchunguza makontena 277 ya mchanga wa madini yaliyozuiliwa kusafirishwa kugundua kuwa kuna madini mengi yanapitishwa kwenye mchanga huo.

Waziri Mwijage ambaye katika Serikali ya Awamu ya Nne aliwahi kuwa Naibu Waziri Katika Wizara ya Nishati na Madini atakuwa na kazi nzito katika bajeti hii kutokana na sakata la mchanga huo ambao wabunge wamekuwa na maoni tofauti tangu Rais Magufuli alipochukua uamuzi wa kuzuia makontena hayo.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: