
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi π΅πͺπ΅πͺ
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
TAKUKURU imesema inawashikilia Harbinder Singh Sethi na Jemes Rugemalila kwa makosa ya uhujumu uchumi. Wanapelekwa kwenye mahakama ya kisutu na baadae watapelekwa Mahakama ya Maalumu ya kifisadi
"Ndugu wanahabri, leo tumekutana tena mchana huu, ili kuwapeni taarifa za Mapambano yetu dhidi ya rushwa na Ufisadi nchini. Na leo tunawapa taarifa kwamba tunawafikisha mahakamani watuhumiwa wawili, Bwana Harbinder Singh Sethi na bwana Jemes Rugemalila. Hawa tunawafikisha mahakamani kwa Kosa la uhujumu Uchumi na makosa mengine yanayofanana na hayo. Kwa muda mrefu sana nmekuwa naulizwa, Kesi za Escrow zimeishia wapi, Kesi ya IPTL imeishia wapi. Kama tulivyowahi kusema Mwanzo kwamba Taasisi ya kuzuia na kupambana na ruswa, inajukumu la kimsingi la kupambana na rushwa na makosa ya ufisadi. Kwahiyo katika muendelezo wa majuku yetu,tulichunguza shauri hili kwa muda mrefu, Sasa imefika muda muafaka wa kuwafikisha watuhumiwa wakuu hawa wa mashauri hayo ya uhujumu uchumi wa nchi yetu mahakamani.
Kwa hiyo tayari wameshapelekwa mahakamani, na nitoe wito kwa wananchi kwamba Serikali ina nia ya dhati ya kupambana na vitendo vya uhumumu uchumi wa Nchi yetu ili wananchi wapate maisha bora zaidi. Na jukumu hili TAKUKURU itaendelea kulitekeleza kwa nguvu zetu zote, kwa waledi wetu wote na kwa umakini wa hali ya juu ili kuhakikisha kwamba vitendo vya hujuma dhidi ya uchumi wa nchi yetu vinadhibitiwa ili wananchi wapate Maisha Bora".
Post A Comment: