ads

Muigizaji nguli, Sylvester Stallone anayefahamika pia kwa jina la filamu yake ya ‘Rambo’, ametoa maoni yake kuhusu pambano kati ya bingwa wa zamani wa dunia ambaye hajawahi kushindwa, Floyd Mayweather na bingwa wa mapambano ya UFC, McGregory.


Stallone ameonesha kushangazwa na uandaaji wa pambano hilo akidai kuwa hawakutenda haki kwani anaamini baada ya pambano hilo Mayweather atakuwa akikabiliwa na kesi ya mauaji.

“McGregory ni mpiganaji mzuri na shupavu kwenye ulingo wake (UFC). Lakini Mayweather atakuwa anakabiliwa na kesi ya mauaji baada ya pambano hilo kwa mara ya kwanza. Sio haki,” alisema Stallone.

Aliongeza kuwa waandaaji wa pambano hilo walimpigia simu kabla wakitaka maoni yake kuhusu pambano hilo, lakini aliwajibu kuwa haitakuwa haki hata kidogo kumkutanisha bingwa wa masumbwi duniani ambaye ni ‘genius’ na mtu ambaye hana ujuzi wa mchezo huo.

Alisisitiza kuwa ana heshimu sana uwezo mkubwa wa McGregory na ushupavu wake, lakini ni jambo la ajabu kumkutanisha na Mayweather kwenye ulingo wa ndondi na wakategemea atafanya kitu cha ajabu.

Mayweather na McGregory wanatarajia kupanda ulingoni August 26 mwaka huu kukata mzizi wa fitina, Las Vegas, Marekani, pambano ambalo limeandaliwa na kampuni ya Mayweather (Mayweather Promotion).
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: