Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, amemshukuru Rais Magufuli kwa kumteua kuwa mkuu wa mkoa huo, huku akisema kuwa yeye sio mpinzani wa maendeleo.


Bi Anna Mghwira amesema hayo wakati wa hafla ya kuapishwa iliyofanyika leo, Jumanne jijini Dar es salaam na kuhudhuriwa na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa.

“Ninasema hii ni heshima kwa Taifa letu, ni heshima kwa umoja wa nchi yetu, ni heshima kwa siasa za umoja wa nchi yetu, kumekuwa na minong’ono mingi sana kuwa Rais analeta nini, kuteua watu wanaitwa wapinzani, mimi sio mpinzani wa maendeleo,” amesema Mghwira.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: