ads

Mjasiriamali na mwanamitindo maarufu nchini Tanzania, Jokate Mwegelo amedai kitu ambacho kimemtoa machozi hivi karibuni ni jinsi mama yake anavyotumia nguvu kubwa kumuuguza baba yake ambaye anaumwa kwa muda mrefu.


Mrembo huyo ambaye ametajwa katika orodha la jarida la Forbes Africa la kuwa miongoni mwa vijana walio na umri chini ya miaka 30 wenye mafanikio mbalimbali kwa mwaka 2017, alisema hayo baada ya kuulizwa ni kitu gani hivi karibuni kimemtoa machozi.

“Kusema kweli hivi karibuni nimelia sana, baba yangu anaumwa sasa mama yangu anatumia nguvu kubwa kumuudumia kwa sababu baba anahitaji uangalizi wa karibu sana,” Jokate aliimbia MCL.

Pia mwanamitindo huyo amedai kwa sasa anatamani kuwa na familia lakini bado hajajua ni lini.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: