ads

MBUNGE wa Ukonga, Mwita Waitara (Chadema), amesema wananchi wamewageuza wabunge wa Tanzania na kuwa kama mashine za kutolea fedha (ATM) na Vyama vya Kuweka na Kukopa (SACCOS).


Kutokana na hali hiyo, amesema kuna haja Serikali kuboresha mafao yao ili yaendane na majukumu wanayokabiliana nayo.

Waitara aliyasema hayo jana mjini hapa wakati wa semina ya wabunge walioko katika mabunge ya nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola (CPA).

“Mshahara wa mbunge kila mwezi unakatwa shilingi milioni 1.2, lakini baada ya kumaliza miaka mitano ya ubunge, mafao yake yanakatwa tena.

“Hivi huo utaratibu mliutoa wapi wakati haupo nchi yoyote duniani? Sisi wabunge tumegeuzwa kama ATM au saccos kwa sababu tutatoa pesa kila mahali.

“Kule Kenya ofisi ya mbunge ni kama taasisi kwa sababu ina mbunge na ina mtafiti anayemsaidia mbunge kila anapotaka kufanya mambo yake.

"Hata kukiwa na harambee, mbunge unaitwa na kutakiwa uchangie fedha nyingi, sasa utachanga kwa fedha zipi wakati mnatulipa kidogo, yaani huu ni mzigo kwetu wabunge.

“Kwa hiyo, tuongezeeni mafao kwa sababu tunalipwa kidogo sana ikilinganishwa na nchi zingine,”alisema Waitara.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: