ads

Rais mpya wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Ahmad Ahmad amekataa kupokea mshahara wake kutoka kwa shirikisho hilo.


Akitoa sababu za kukataa kupokea mshahara huo, Ahmad alisema kuwa shirikisho hilo haliheshimu uongozi au utawala bora na haki za wafanyakazi.

“Nimekataa mshahara wa CAF kwa sababu rahisi, haiheshimu utawala bora. Mishahara ya waajiriwa wote wa CAF, kuanzia ngazi ya uongozi hadi kwenye Kamati na rais mwenyewe, kote inapaswa kuwe na uwazi,” Ahmad ameiambia BBC.

Ahmad ambaye ni raia wa Madagascar ameweka wazi msimamo wake kuhusu mshahara, wakati ambapo anafanya mkutano wake wa kwanza leo na viongozi waandamizi wa CAF kabla ya kushiriki mkutano wa Shirikisho la Soka Duniani (FIFA), utakaofanyika Alhamisi ya juma hili.

Ajenda kubwa ya mkutano wa leo ni namna ya kufanya mageuzi ya kiutawala katika shirikisho hilo.

Ahmad aliingia madarakani mwezi Machi kupitia uchaguzi, baada ya kumwaga Issa Hayatou’s aliyeongoza kwa takribani miongo mitatu.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: