ads

Madaktari watalii waliotoa msaada wa awali baada ya ajali iliyowaua wanafunzi na waalimu wa Lucky Vicent Academy wameahidi kuwapatia msaada majeruhi watatu waliobaki hospitalini hata kuwapeleka nje ya nchi kama itahitajika.


Akiwaongoza wakazi wa Arusha kuomboleza msiba katika viwanja vya Sheikh Amri Abeid, Makamu wa Rais, Mh. Samia Suluhu amesema kwamba Madaktari hao walikuwa watalii na gari lao lilikuwa mbele ya 'bus' la wanafunzi na hata baada ya ajali kutokea wao ndio walikuwa watu wa kwanza kutoa msaada wa kitaalamu.

Katika hotuba yake Makamu wa rais amesema kuwa hata baada ya kutoa msaada watalii hao  kutoka shirika la afya nchini Marekani wameahidi kujitolea kuwapatia matibabu wanafunzi watatu ambao ni majeruhi wa ajali hiyo na hata msaada kutoka nje ya nchi  wapo tayari kututoa.

ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: