
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
RAIS Dk. John Magufuli amesema serikali itawachuguza na kuwachukulia hatua baadhi ya wafanyakazi ambao wamebadili umri wao ili waendelee kuwepo kwenye ajira serikalini.
Akizungumza jana kwenye sherehe ya sikukuu ya wafanyakazi dunia zilizofanyika kitaifa kwenye viwanja vya Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi mkoani Kilimanajaro, alisema wapo wafanyakazi ambao wamebadilisha umri wao na wanaendelea kuwepo kwenye ajira licha ya kwamba wamezeeka na walistahili kustaafu.
“Wapo watumishi ambao wamebadilishi umri wao wa kuishi wamebadilisha miaka yao, unakuta ni mzee kabisa lakini yeye hastaafu tu huyo naye hana utofauti sana na mfanyakazi hewa, kwa sababu ameshamaliza muda wake hataki kutoka kazini awaachie wengine nao wafanye kazi anaendelea kukaa pale kubadilisha miaka,”alisema.
“Mimi hapa nilipo nilikuwa nimebakiza miaka miwili tu kustaafu lakini hebu kaangalieni kwenye maofisi yenu wapo watu ambao ni wazee kuliko mimi bado wanafanya kazi na wanasema ndio wakati umefika, hawa nao dawa yao tunaichunguza” Rais Magufuli alisema kimsingi kazi ya kuondoa wafanyakazi hewa imeenda vizuri na limefikia asilimia 98 lakini bado halijaisha.
Aliongeza kuwa katika fedha tu za watumishi hewa, ukichukulia tu mshahara serikali ilikuwa inapoteza Sh. bilioni 19.8 kwa mwezi na kwa mwaka ni zaidia Sh. Bilioni 230.
Post A Comment: