ads

Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kwa tiketi ya CHADEMA Mhe. Godbless Lema ametoa masikitiko yake na kuonyesha kuumizwa na kitendo alichofanyiwa leo wakati wa kuaga miili ya wanafunzi, walimu na dereva waliofariki katika ajali ya basi.


Lema anasema kitendo cha yeye kama Mbunge wa Arusha mjini pamoja na Meya wa jiji kunyimwa nafasi japo ya kutoa pole kwa familia na wafiwa wakati wa kuaga miili hiyo ni ubaguzi mkubwa. 

"Ninamshukuru Makamu wa Rais kuja kutoa pole kwa watu wa Arusha. Leo ni ubaguzi mwingine katika Taifa Mbunge na Meya kwa kunyimwa nafasi ya kutoa pole" alisema Goodbless Lema 


ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: