ads

Rapa Dogo Janja amefunguka na kusema msanii kutoka Nigeria Davido licha ya kuwa na pesa nyingi lakini msanii huyo hajui kabisa kupendeza kwani mara nyingi hata nguo anazovaa ni kama zimetundikwa tu mwilini mwake.


Dogo Janja anasema wapo watu wengine wanapesa nyingi lakini suala la kuvaa kwao ni zero na kumtolea mfano Davido kuwa ni moja ya watu ambao wanapesa nyingi lakini hajui kuvaa na hata nguo akivaa zinakuwa hazimkai vizuri mwilini. 

Mbali na hilo Dogo Janja alikwenda mbali na kusema kwa bongo yeye ndiye anakamata nafasi ya kwanza kwa uvaaji kwa wasanii huku akisema msanii mwingine ambaye amekuwa akijitahidi tahidi kwa mitupio kuwa ni G Nako, Jux kwa mbali na Joh Makini.  

Janjaro aliendelea kusema kuwa wasanii wengi wa bongo wamekuwa wakivizia nguo za kutungua Kariako ndiyo maana hawawezi kushindana na yeye kwa kuwa yeye nguo zake anaagiza kutoka nje ndiyo maana anaonekana tofauti na wao katika uvaaji na kupendeza. 
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: