ads

Mbunge wa Kigoma mjini kwa tiketi ya ACT Wazalendo Mhe. Zitto Kabwe amefunguka na kusema bei ya unga wa ugali sasa ni juu kuliko hata bei ya mafuta ya magari jambo ambalo linafanya wananchi kuumia na gharama hizi za chakula.


Zitto Kabwe amesema hayo kupitia mtandao wake wa Facebook na kusema bei hizi za chukula zipo juu sana na kufanya wananchi kuingia kwenye umasikini  

"Bei ya Unga wa Sembe 1kg TZS 2,300/= ( wastani ). Bei ya Mafuta ya Petroli 1lita TZS 2,060/= ( wastani). Kwa mara ya kwanza Ugali umekuwa ghali kuliko mafuta ya gari. Gharama hizi za maisha Kwa wananchi ni kubwa mno, hazistahmiliki na zinaingiza raia wengi kwenye umasikini. Serikali ipo kimya kana kwamba kila kitu kipo sawa" alisema Zitto Kabwe 
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: