ads

KATIKA kutekeleza agizo la Rais John Magufuli, uongozi wa Jiji la Arusha umeanza mchakato wa kujenga jengo la kufanyia shughuli za biashara wafanyabiashara wadogo maarufu ‘Wamachinga.’


Eneo lililotengwa kwa mradi huo lipo katikati ya Jiji, kwenye kiwanja Namba 69 chenye ukubwa wa zaidi ya ekari moja, sehemu ambayo ilirejeshwa serikalini na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati wa ziara yake mkoani Arusha hivi karibuni.

Kiwanja hicho kilichopo mkabala na soko la Kilombero, linadaiwa awali liliuzwa kinyemela na madiwani wa halmashauri, kabla ya Waziri Mkuu kuamuru lirudishwe na tayari eneo hilo limerudi serikalini.

Akizungumzia hilo, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Arusha, Athumani Kihamia alisema eneo hilo lina uwezo wa kuhifadhi wafanyabiashara wadogo zaidi ya 2,000 pamoja na shughuli mradi utakapokamilika. Jiji la Arusha lina wakazi takribani 500,000.

Mmoja wa machinga anayeuza viatu, Hussein Issa, amesema hilo ni jambo jema, huku akushauri kusiwe na urasimu wakati wa ugawaji wa maeneo yaliyotengwa kwa ajili yao.

DOWNLOAD APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD BONYEZA HAPA  

ANDIKA MAONI YAKO HAPO CHINI
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: