MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameagiza kuchunguzwa kwa
sukari kontena 115 ambayo ni zaidi ya tani 3,000 iliyokutwa katika
bandari kavu ya PMM iliyopo eneo la Vingunguti.
Makonda alitoa agizo hilo jana wakati alipofanya ziara ya kushtukiza
katika bandari hiyo na kubaini uwepo wa sukari hiyo ambayo ni mali ya
Mohamed Enterprises, ambayo kwa taarifa zake aliambiwa zilikuwa kontena
165.
Alisema anazitaka mamlaka zinazohusika kama Mamlaka ya Chakula na
Dawa (TFDA), Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), pamoja
na Shirika la Viwango (TBS) kuichunguza sukari hiyo kutokana na sababu
mbalimbali zilizojitokeza katika uwepo wa sukari hiyo kama sukari
kuagizwa kutoka Dubai lakini imetoka Brazil na imepakiwa Dubai, na
upangwaji wa kontena hizo katika bandari hiyo.
“Nashindwa kuelewa kwa nini sukari iagizwe kutoka Dubai lakini itoke
Brazil na kufungashwa Dubai inaonesha inaweza kuwa imeshawahi kuisha
muda wake hivyo nataka ichunguzwe na tunataka tujue kama Mohamed
Enterprises anaficha sukari ili ipelekwe kwa wananchi kwa matumizi,”
alisema Makonda.
Mbali na kutoa maagizo hayo, Makonda pia amezuia kutumika kwa sukari
mifuko 22,000 iliyokutwa katika ghala la Mohamed Enterprises Tanzania
Limited (MeTL) lililopo Barabara ya Nyerere na kutaka wapeleke vielelezo
kuhusu sukari hiyo kwa mamlaka zinazohusika kama ya matumizi yoyote.
DOWNLOAD
APP YETU YA SWAHIBA NEWS ILI UWEZE KUPATA HABARI ZOTE MOJA KWA MOJA
KUPITIA SIMU YAKO YA MKONONI BILA KUINGIA KWENYE WEBSITE,KUDOWNLOAD
BONYEZA HAPA



Post A Comment: