ads
Tetesi za usajili ndani ya klabu ya Yanga zinasema kwamba, mshambuliaji wake, Rais wa Liberia, Kpah Sherman anakaribia kutua katika klabu mojawapo inayoshiriki ligi kuu nchini Afrika Kusini.
Winga aliyekosa nafasi katika kikosi cha kwanza cha  Yanga, Mbrazil,  Andrey Coutinho anatafutiwa timu itakayomnunua baada ya BDF XI ya Botswana kutaja pesa dau dogo la milion 10 za Kitanzania. Hata hivyo St.George ya Ethiopia wameonesha kuvutiwa na Coutinho.
Yanga imepanga kumalizana na kiungo mkabaji wa Gor Mahia , Khalid Auch pamoja na mshambuliaji Michael Olunga ambaye Azam FC na Simba SC wanawania saini yake pia.
Beki kiraka, Mbuyu Twite yupo mashakani kuendelea kukipiga Jangwani huku tatizo haswa imekuwa usumbufu kutoka klabu yake ya zamani ya FC LUPOPO.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: