ads

Raia wa Colombia, Sandar Milena (30) ametafuna na kumeza Yuro 7,000 sawa na Sh17 milioni alizokuwa ameweka akiba baada ya kugunduwa mumewe ana mchepuko.


Imeelezwa kuwa Milena amefanya hivyo kwa makusudi ili mumewe asizitumie na mchepuko wake.

Hata hivyo baada ya kutafuna na kumeza noti moja baada ya nyingine, Milena aliumwa na tumbo na kukimbizwa hospitali.

Kwa mujibu wa shirika ya utangazaji la BBC ni kuwa Milena alifikishwa hospitalini na kufanyiwa upasuaji.

Mkurugenzi wa upasuaji katika hospitali ya Chuo Kikuu cha Santander, Juan Serrano amesema Milena alifanyiwa upasuaji na fedha hizo zikatolewa.

“Alifanya hivyo kutokana na tatizo lililomkabili ila tumefanikiwa kutoa baadhi noti zikiwa nzima  katika utumbo mkubwa lakini  nyingine zimeharibika,”amesema.

Mkurugenzi huyo amesema Milena anaendelea vizuri na afya yake inatarajiwa kuimarika zaidi.


ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: