ads

Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA), imesema hali ya vipindi vifupi vya mvua katika maeneo ya mwambao wa pwani ya Kaskazini itaendelea hadi Mei 9.


Taarifa ya tahadhari iliyotolewa na TMA leo saa tisa alasiri inasema kunatarajiwa kuwapo vipindi vifupi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24. Mamlaka hiyo imesema maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni mikoa ya Tanga, Dar es Salaam na Pwani. Pia, visiwa vya Unguja na Pemba.

TMA imesema hali hiyo inatokana na kuimarika kwa ukanda wa mvua katika ukanda wa Pwani ya Kaskazini.

“Wakazi wa maeneo tajwa wanashauriwa kuchukua tahadhari na hatua stahiki. Mamlaka inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejeo kila itakapobidi,” imesema taarifa ya TMA.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: