ads

MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini, Abdulaziz Chande ‘Dogo Janja’, amewaangalia wanamuziki wenzake wote na kubaini hakuna anayemgusa kwa kupiga pamba.


Dogo Janja amesema kwamba, moja ya siri ya mafanikio yake ni kuvaa kwani hali hiyo imekuwa ikumuongezea ushawishi mkubwa kwa jamii inayomzunguka.

Alisema amekuwa akitumia gharama kubwa kujiweka nadhifu na hajutii gharama anazotumia kwa kuwa ameendelea kuwafunika wasanii wenzake kwa upande wa mavazi.

“Unajua moja ya mafanikio niliyonayo kwenye muziki ni pamoja na upigaji wangu wa pamba ambao umekuwa ukinigharimu pesa nyingi, lakini sijawahi kujutia kwa sababu nimewafunika wasanii wenzangu wote,” alisema Dogo Janja.

Aidha, msanii huyo kwa sasa ameingia kwenye ushindani na msanii mwenzake, Juma Jux ambaye ni miongoni mwa wasanii wanaodaiwa kutupia pamba kali zaidi.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: