
Subscribe ndio neno gumu zaidi kwa wabongo kuliko kutafuna jiwe kama ilivyo kwa Waingereza kutamka Mwanjelwa..husema Monjela
Pamoja na vionjo hivyo..kwenye Simba Day ya mwaka huu ntakuja na style tofauti ya kutambulisha wachezaji...njoo ushuhudie mwenyew..usingoje kuhadithiwa ni Jtano hii pale dimba la Taifa... #SimbaDay #KibingwaZaidi 🇵🇪🇵🇪
Serikali yatoa tamko kuadimika mafuta ya kula nchini
Waziri Kigwangalla atetea ununuzi wa ndege
Zitto Kabwe amshauri Job Ndugai
Bunge lataka tende zifutwe kodi mfungo wa Ramadhani
Mo Dewji afunguka jinsi anavyopiga pesa kupitia kilimo
Dunia ina mambo, na ukiyashangaa haya jiandae kuyastaajabia yajayo..!
Mwanaume mmoja aliyejitambusha kwa jina la Aaron Chervenak mwenye umri wa miaka 34 na mkazi wa Los Angeles nchini Marekani, amefanya tukio la aina yake baada ya kufunga ndoa kanisani na simu yake ya kupapasa (smartphone).
Mwanaume huyo alisafiri hadi Vegas kulisaka kanisa moja ambalo lilimkubalia kufunga ndoa na simu yake na kula kiapo kama ambavyo alipaswa kula kiapo kwa mrembo aliyeyagusa maisha yake na kuamua kumfanya mkewe wa maisha.
Akizungumzia sababu zilizopelekea yeye kufanya tukio hilo, kupitia makala maalum ya ndoa yake hiyo, Aaron alisema kuwa ameamua kufanya hivyo kwa sababu ya ukweli kwamba simu zimekuwa zikichukua nafasi kubwa ya mapenzi na uhusiano na zikifanya jukumu kubwa la kuwatuliza watu katika dunia hii.
“Kama tutakuwa wakweli, tunaunganishwa na simu katika viwango vingi vya hisia. Tunaikimbilia kututuliza, kutulaza usingizi, kuweka unafuu kwenye mawazo yetu. Na kwangu, huo ndio uhusiano nilionao na simu yangu hii,” alisema Aaron.
“Kwa mantiki hiyo, simu yangu hii imekuwa na uhusiano wa muda mrefu na mimi na ndio maana nimeamua kufunga nayo ndoa,” aliongeza.
Kuhusu jinsi alivyokubaliwa kufanya tukio hilo kanisani, alisema kuwa alijaribu kuwasiliana na uongozi wa kanisa hilo kuona kama angeruhusiwa lakini alihakikishiwa kuwa anakaribishwa kwa mikono miwili.
Post A Comment: