ads

MFANYABIASHARA maarufu nchini Tanzania, Mohammed Dewji ambaye ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group amefunguka na kuwapa siri vijana wa Tanzania kuwa wanapaswa kujikita zaidi katika kilimo kwani ndipo sehemu ambayo ina pesa nyingi sana.


Dewji alisema hayo alipokuwa akifanyiwa mahojiano na moja ya kituo cha habari na kusema kuwa yeye anatengeneza fedha nyingi zaidi kupitia kilimo ambacho anakifanya na kwamba anatengeneza faidi kubwa kupitia kilimo cha chai, korosho na katani. 

“Niwambie siri moja vijana wenzangu kuna pesa nyingi sana kwenye kilimo, mimi nipo kwenye kilimo nipo kwenye katani, nipo kwenye chai, nipo kwenye korosho na ninatengeneza fedha nyingi sana kupitia kilimo” alisisitiza Mo Dewji.

 Mbali na Mohammed Dewji watu wengine maarufu ambao wamejikita kwenye kilimo ni pamoja na Rais mstaafu wa awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu wa awamu ya nne Mhe. Mizengo Kayanza Pinda, Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa na Mwenyekiti wa CHADEMA Mhe. Freeman Mbowe.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: