ads

 Mbunge wa zamani wa Muhambwe (NCCR-Mageuzi), Felix Mkosamali amekanusha taarifa zilizosambaa katika mitandao ya kijamii kuwa amejivua uanachama wa chama hicho na kujiunga na CCM.


Mkosamali amesema ana imani na upinzani imara. Ametaka kupuuzwa kwa taarifa kuwa anakwenda CCM kuunga mkono jitihada za Rais John Magufuli.

“Msimamo  wangu upo palepale na kama wamezusha ni wao na sababu zao. Watu wamenipigia simu kuniuliza kuhusu jambo hili. Sijaeleza lolote kuhusu kuhama NCCR. Watanzania tunahitaji upinzani imara, kuhama hatumsaidii Rais unaweza kumsaidia ukiwa hukuhuku upinzani,” amesema.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: