ads

Simba imefanya usajili wa kishindo katika dakika za mwisho kwa kuwasajili wachezaji wawili wa kimataifa Asante Kwasi na Domingos Anthonio.


Simba imempa mkataba ya miaka miwili beki Mghana Kwasi akitokea Lipuli pamoja na Domingos akitokea Ferroviario de Beira ya Msumbiji

Mbali ya kuwasajili nyota hao katika usiku huo wa Desemba 15, vinara hao wa Ligi Kuu Bara wameacha wachezaji watatu kati ya hao wawili wa kigeni na mmoja mzawa.

Mshambuliaji Laudit Mavugo ametolewa kwa mkopo katika ligi kuu ya nchini Oman, pia Jamal Mnyate amejiunga Lipuli kwa mkopo wakati nahodha Mzimbabwe Method Mwanjali akiachwa kutokana na kusumbuliwa na majeruhi. 
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: