ads
Watu wawili wamefariki dunia akiwemo askari wa Jeshi la wananchi (JWTZ) na wengine 33 kujeruhiwa baada ya basi mali ya kampuni ya Ngorika kuigonga kwa mbele Toyota Costa eneo la Misugusugu mjini Kibaha .

Ajali hiyo imetokea majira ya saa 1.30 asubuhi Jana wakati basi hilo likitokea Dar esalaam kwenda Arusha ambapo ilipofika eneo hilo dereva alihama upande wake wa njia kuyapita magari mengine yaliyokua mbele yake bila tahadhali hivyo kwenda kugongana uso kwa uso na costa iliyokua ikitokea Miono Bagamoyo kwenda Dar esalaam.

Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Jafari Mohamed amethibitisha tukio hilo na kutaja waliokufa ni Rutta Saimon mwalimu wa shule ya msingi Mwambao Bagamoyo na Peter Maro askari wa JWTZ na kwamba anasadikiwa kuwa ni wa Kikosi cha Jeshi la Nyumbu Kibaha na wote walikua abiria katika Costa hiyo.

Kamanda Jafari amesema kati ya majeruhi hao 33, wanne hali zao ni mbaya kutokana na kuvunjika sehemu mbalimbali za mwili.

"Majeruhi wote wa ajali hiyo walipelekwa Tumbi na walitibiwa na wengi wao wameruhusiwa kuendelea na safari yao lakini hao wanne ndiyo wamelazimika kulazwa hapo kwa matibabu zaidi kutokana na hali zao kuwa mbaya maana wamevunjika sehemu mbalimbali za mwili, na pia miili ya marehemu imehifadhiwa hospitalini humo kusubiri ndugu"amesema Kamanda Jafari.
ads
Bonyeza HAPA kudownload applicationi ya SWAHILI NEWS kwenye simu yako ili kupata habari zetu Haraka
Share To:

SWAHIBA MEDIA STAFF

Habari , karibu katika mtandao wetu ili kuhabarika na stori zote za siku katika lugha yetu adhwim ya kiswahili, habarika wakati wote weka dunia kiganjani mwako na swahili news

Post A Comment: